1 Chronicles 14:1-6

Nyumba Ya Daudi Na Jamaa Yake

(2 Samweli 5:11-16)

1 aBasi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme. 2 bNaye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.

3 cHuko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi. 4 dHaya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Sulemani, 5Ibihari, Elishua, Elpeleti, 6Noga, Nefegi, Yafia,
Copyright information for SwhKC